Kasisi badia ajipenyeza mkutano wa makadinali



Mtu aliyejifanya Kardinali wa Kanisa Katoliki, Ralph Napierski (kushoto) akisalimiana na Kardinali Sergio Sebiastiana. Napierski alikamatwa akijaribu kuingia kwenye mkutano wa makardinali unaoendelea Vatican
Vatican, Italia
Askofu bandia amefanikiwa kujipenyeza na kuingia kwenye mkutano wa makadinali unaoendelea mjini Vatican, kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi wa Papa mpya.
Askofu huyo bandia, Ralph Napierski ambaye ni mzawa wa Ujerumani alifanikiwa kujipenyeza na kusalimiana kisha kupiga picha za kumbukumbu na baadhi ya makadinali waliopo kwenye mkutano huo bila kugundulika.

Uzamiaji wake ambao ulileta mashaka kuhusu uimara wa usalama eneo hilo wanapokutana makadinali 103, ambao wamekusajika kwenye Makao Makuu ya Kanisa Katoliki kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi wa Papa mpya, huku wengine 12 wakiwa hawajawasili.

Katika mkutano huo, Kadinali wa juu kutoka Uingereza, Cormac Murphy O'Connor pia anahudhuria.
Napierski alionekana akisalimiana na Kadinali Sergio Sebiastiana nje ya ukumbi wa Papa Paul VI akiwa hajatambua kuwa siyo miongoni mwa wenzake, huku akiwa amezungukwa na makasisi wengine wa kanisa hilo ambao pia hawakuweza kutambua.

Walinzi wa kundi la Swiss Guars linaloshughulika na ulinzi wa Makao Makuu ya Kanisa Katoliki Vatican, walimbaini kuwa siyo miongoni mwa wahusika kutokana na vazi lake alilofunga kiunoni, ambalo siyo sahihi bali ulikuwa ni mtandio uliokunjwa vizuri.

Pamoja na vazi hilo la rangi ya zambarau kutokuwa sahihi, pia kofia aliyokuwa ameivaa haikuwa miongoni mwa zile zinazotambulika kuvaliwa na viongozi wa kanisa hilo.
Tofauti nyingine iliyobainika ni ufupi wa kanzu yake na rozari aliyovaa haikuwa halisi, kwa kuwa ilikuwa ni fupi kuliko wanazotumia viongozi wa kanisa hilo.

Kabla ya kubainika, Napierski alijitambulisha kwa waandishi wa habari kwamba jina lake ni Basilius ni miongoni mwa wawakilishi wa Kanisa la Orthodox kutoka Italia.

Awali, kulikuwa na taarifa kwamba aliwaeleza waandishi wa habari kuwa Kanisa Katoliki limefanya “Kosa kubwa” kwa kuwaruhusu makasisi wanaotuhumiwa kwa makosa ya ngono kubadilishwa kutoka maeneo yao ya awali na kupelekwa kwingine, kuficha kashfa zao badala ya kuzishughulikia.

Mtuhumiwa huyo ambaye baada ya kubainika aliondolewa eneo hilo, anaongoza tovuti ambayo aliitumia kujitambulisha kwamba yeye ni kasisi kupitia Shirika la Kikatoliki la Corpus Dei, huku akiwa amevaa mavazi ya kikasisi na kujidhihirisha kama “Mtumwa na Nabii kama Mtakatifu Paul”.

Msemaji wa Kanisa Katoliki mjini Vatican, Federico Lombardi alisema hayupo tayari kuzungumzia suala hilo kwa sababu hajapata taarifa yoyote na muda wote alikuwa akishughulika katika mkutano 

MHARIRI MKUU NA MWENYEKITI WA JUKWAA LA WAHARIRI ABSALOM KIBANDA AVAMIWA USIKU WA MANANE NA KUJERUHIWA VIBAYA



Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya New Habari wachapishaji wa magazeti ya Mtanzania, Dimba, Bingwa na Dimba, Absalom Kibanda amevamiwa na watu wasiojulikana akiwa ndani ya gari lake wakati akiingia nyumbani kwake Mbezi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

Kibanda alivamia majira ya saa sita usiku wa kumkia leo, akitokea kwenye majukumu yake ya kila siku. Inadaiwa kuwa alichomolewa kwene gari, akapigwa na vitu vyenye ncha kali kichwani, ametobolewa jicho lake la kushoto pamoja na kunyofolewa kucha na baadhi ya vidole na hatimaye kutupwa umbali kidogo ya nyumbani kwake. 

Baada ya hapo wasamalia wema walijitokeza na kumkimbiza Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, ambako alipokelewa vizuri na madaktari na kumpatia tiba ya awali na baadaye kumhamishia Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) ambako mpaka sasa anaendelea na matibabu. 

Watu waliomfanyia madhara hayo, hawakuweza kuchukua kitu chochote kwenye gari ambapo kulikuwemo Laptop, simu na nyaraka zingine. 

Blog ya Kamanda wa Matukio imesikitishwa sana na unyama huo aliofanyiwa mpiganaji Kibanda na inaomba vyombo vya Dola vifanye jitihada za ziada kuwabaini wale waote walihusika na kuwafikisha kwenye mikono ya sheria. 

Pole saaaana mpiganaji wetu Kibanda, Mungu atakujalia upate matibabu na kupona haraka. Amin.

RAIS HUGO CHAVES AFARIKI DUNIA

Mamia ya wavenezuela walikusanyika mbele ya hospitali ambapo kiongozi wao Hugo Chavez alifariki jana kutokana na ugonjwa wa kansa.

Miongoni mwao walionekana wakipepea bendera za Venezuela huku wengine wakiwa na mabango yenye maandishi, “People, Chavez and revolution, the battle continues”, na kusikika watamka “Chavez lives”. Rais huyo amefariki akiwa na umri wa miaka 58.

Kutokana na kifo hicho, serikali imetenga siku saba za maombolezo ya kitaifa. Wananchi wengi wamekusanyika kwenye maeneo ya wazi kwenye mji mkuu Caracas na miji mingine wakiimba wimbo wa taufa, wakibubujikwa na machozi na kushika picha za kiongozi huyo.

“Asingefariki. Alikuwa rais bora kuwahi kutokea Venezuela,” alisema Frank Aponte, 45, aliyekuwa kwenye mtaa mmoja wa Caracas. Shughuli za kuuaga mwili huo mbele ya viongozi wengine wa kimataifa zitafanyika Ijumaa.

Katiba ya nchi hiyo inasema uchaguzi lazima ufanyike ndani ya siku 30 tangu kifo cha rais lakini serikali bado haijatangaza tarehe.

CHADEMA YABADILI MBINU ZA KUWANIA IKULU 2015. PIA YAZINDUA M4C JIMBO LA MBEYA




Mwenyekiti wa Chadema taifa, Freeman Mbowe akiongea na viongozi wa Chadema wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini katika ukumbi wa mkapa jijini Mbeya












Maandamano ambayo yaliongozwa na Mbowe yaliyoanzia katika eneo la Uhasibu Mafiat hadi katika Uwanja wa Ruanda Nzovwe,Mbowe aitembea kwa mwendo wa kilomita tano ambapo makundi ya waendesha bodaboda, baiskeli na watembea kwa miguu walijitokeza kwa wingi kuunga mkono maandamano hayo.









CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimesema kuwa kitalazimisha maandamano nchi nzima iwapo Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Naibu wake hawatakubali kujiuzulu kwa kusababisha anguko la elimu nchini.













CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema kuwa kimeamua kuanza kutekeleza sera yake ya kuongoza kwa majimbo sasa ili kuongeza nguvu ya mapambano na harakati za kuhakikisha wanafanikisha malengo yao ya kushika dola mwaka 2015, badala ya kuendelea kutumia mfumo wa zamani ambao ilikuwa rahisi kudhibitiwa na serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) .


Kadhalika, chama hicho kimesema hakitampokea mwanachama yeyote wa Chama Cha Mapinduzi atakayekosa nafasi ya kugombea kwenye chama chake na kutimkia Chadema katika dakika za mwisho kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015.


Mwenyekiti wa Chadema taifa, Freeman Mbowe aliyasema hayo wakati akizungumza na viongozi wa Chadema wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ikiwa ni maandalizi ya kuzindua kanda yake kwenye kanda hiyo.


Alisema kuwa mfumo wa zamani ambao mambo yote ya harakati za chama hicho yalianzia makao makuu ya chama, ulikuwa ni rahisi kudhibitiwa na dola ya CCM kwa kuwa walikuwa wakiwavizia viongozi wa kitaifa wanapotoka nje kwenda kuendesha harakati wanawapiga mabomu, kuwakamata na kuwafungulia kesi mahakamani.


“Tunataka dola ikusubiri viongozi wa kitaifa watoke makao makuu ili wawadhibiti, wasikie mapambano yanatokea kwenye kanda zetu kama hii ya Nyanda za Juu Kusini, kanda ya Magharibi na nyinginezo,” alisema Mbowe.


Alisema kuwa katika mabadiliko hayo pia Chadema inaachana na siasa za kiuanaharakati na badala yake inaanza kujikita kwenye siasa za maandalizi ya kushika dola.


Akizungumzia utaratibu wa baadhi ya wanachama wa vyama vingine, kikiwemo chama tawala CCM kukimbilia ndani ya chama hicho baada ya kutoswa kwenye nafasi za uchaguzi, Mbowe amesema kuwa kuanzia sasa Chadema hakitampokea mwanachama yeyote wa aina hiyo.


Mbowe alisema kuwa Chadema hivi sasa ipo kwenye maandalizi makubwa ya kunyakua dola mwaka 2015 na hivyo inao wajibu wa kuwaandaa wanachama wake ipasavyo ili kiweze kuwa na wagombea wazuri, imara na wenye uwezo wa kuwezesha chama hicho kupata ushindi mkubwa.


“Kama kuna mtu leo anakula matunda ya ufisadi ndani ya Chama Cha Mapinduzi akidhani kuwa atahamia Chadema kwa kuwa ana fedha za kununua kura za maoni, ameula wa chuya, hatutampokea mtu wa aina hiyo, ” alisema Mbowe.


Alisema kuwa kuanzia sasa Chadema itawapokea wanachama kutoka vyama vingine baada ya kuwapima uadilifu wao, kuchunguza historia yao na utayari wao wa kutumika ndani ya chama ili waweze kupata wanachama na viongozi wazuri watakaokisaidia chama kushika dola mwaka 2015.


Alisema kuwa Chama Cha Mapinduzi kimekuwa kikitumia mbinu mbalimbali za kukisambaratisha Chadema, ikiwa ni pamoja na kuwatumia mamluki ndani ya chama, lakini kutokana na uimara wa Chadema mbinu hizo zimekwama na Chadema inasonga mbele.


Mbowe ambaye pia ni kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni alisema kuwa yeye pamoja na wapambanaji wenzake wametumia zaidi ya miaka 20 kuijenga Chadema na kuipa nguvu kisiasa hadi hapo na hivyo hatakubali kuruhusu chama hicho kihujumiwe au kusambaratishwa kwa namna yoyote ile.


Alisema kuwa ikiwa wana-Chadema wataruhusu Chadema ife leo, itawachukua tena miaka 20 mingine kuijenga na kuifikisha mahali iilipo hivi leo.


Mbowe alitolea mfano wa vyama vya siasa vilivyowahi kupata nguvu na umaarufu mkubwa wa kisiasa nchini kama vile Chama cha Wananchi, CUF, NCCR – Mageuzi na TLP ambavyo alidai kuwa CCM illifanikiwa kuvizima na kuwa hata vyenyewe itavichukua muda mrefu usiopungua miaka 20 kurejesha umaarufuvilivyokuwa nao.

Na mbeya yetu

KIJANA ACHOMWA KISU AKITOKA KUPATA STAREHE ZA MWISHO WA WIKI


Kijana Godfrey Masharo mkazi wa mjini Iringa akivuja damu baada ya kuchomwa kisu kifuani na watu wasiofahamika usiku wa leo wakati akitoka kujirusha disco

Hapa akivuja damu akiwa nje ya kituo cha polisi kabla ya kupelekwa hospitali ya mkoa wa matibabu zaidi

Hivi ndivyo alivyochomwa kisu kifuani.

WATU wasiofahamika wamemvamia na kumchoma na kitu chenye ncha kali kifuani mkazi wa mjini Iringa Godfrey Masharo (pichani) .


Tukio hilo limetokea jana usiku majira ya saa 11 alfajiri wakati kijana huyo akitoka kujirusha katika kumbi za starehe mjini hapa.

Akizungumza kwa tabu kijana huyo anadai kuwa watu hao watatu ambao hawafahamiki kwa majina walimvamia na kumchoma na kitu hicho chenye ncha kali kifuani na kukimbia .

Alisema kuwa tukio hilo limetokea eneo la Miyomboni barabara kuu ya Iringa -Dodoma jirani na jengo la Hazina Ndogo ya mkoa wa Iringa .

Hata hivyo alisema kuwa msaada wake ulitoka kwa wasamaria wema ambao walimkuta eneo hilo akiwa ameanguka kwa kupoteza fahamu na kukimbizwa katika kituo cha polisi kabla ya kupelekwa Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa kwa matibabu zaidi .

Je, Kujamiiana Huondoa Msongo wa Mawazo kwa Wanawake?




UTAFITI uliofanywa na Chuo Kikuu cha State cha jijini New York nchini Marekani unaeleza kuwa manii ni nzuri kwa wanawake kwani huwaondolea msongo wa mawazo.
Pia, watafiti hao wamesema wanawake wanaofanya tendo la ndoa mara kwa mara bila kutumia kinga (mapenzi salama) wanakuwa na kiwango kidogo cha msongo wa mawazo na hufanya vizuri katika vipimo vya akili.

Hali hii wamesema wataalam hao kuwa inatokana na manii kuwa na kemikali ambazo humfanya mtu kuwa vizuri kihisia, huongeza upendo/unyenyekevu, huchochea mtu kupata usingizi na huwa na angalau aina tatu za kemikali za kuondoa msongo wa mawazo (anti-depressants).
Utafiti huo uliofanywa kwa kuwahoji wanawake 293 kwa kufuatilia maisha yao ya kujamiana dhidi ya afya za akili zao. Manii huwa na mchanganyiko wa kemikali aina ya cortisol ambayo huongeza upendo, kemikali aina ya esterone na oxytocin ambazo zote humfanya mtu kuwa vizuri kihisia.
Pia, huwa na homoni aina za ‘thyrotropin releasing hormone’, ambayo huondoa msongo wa mawazo, melatonin ambayo huchochea usingizi na serotonin ambayo ni homoni inayoondoa msongo wa mawazo.
Kutokana kuwapo kwa mchanganyiko wa kemikali na homoni hizo kwenye manii
Matokeo ya utafiti

Matokeo muhimu ya utafiti huu ambao umechapishwa katika jarida la ‘Archives of Sexual Behaviour’ ni kwamba hata baada ya baadhi ya watafitiwa kuongeza kiwango chao cha kujamiana, wale ambao walikuwa hawatumii kinga yoyote walikuwa na kiwango kidogo cha msongo wa mawazo tofauti na wale ambao walikuwa wakitumia kinga kama kondomu wakati wa kujamiana.

WEWE UNAYESEMA POLICE TANZANIA NI WAKATILI:JE UMEISOMA HII KUTOKA SOUTH AFRICA:POLICE WAMFUNGA PINGU DEREVA TAX NYUMA YA GARI NA KUMBURUZA BARABARANI


South Africa arrests officers linked to man's dragging death

By Nkepile Mabuse and Faith Karimi, CNN
Watch this video

S. African police violence sparks outrage

Johannesburg (CNN) -- South African authorities Friday arrested eight police officers accused of being involved in dragging a man down a road while he was handcuffed to the back of a police van.
Crowds chased after the van as the man kicked and writhed. He later died.
The incident was captured on video, sparking outrage in a nationthat has seen a series of police brutality incidents recently.
The country's Independent Police Investigation Directorate on Friday arrested the officers, who earlier had been disarmed and suspended, said Zweli Mnisi, spokesman for police ministry.
Tough action will be taken against those involved, the nation's acting police minister said, calling for a speedy independent investigation.
"We view this incident in serious light. We want stern action so that it may send a message to other officers that any untoward conduct will not be tolerated," State Security Minister Siyabonga Cwele said.

Man dragged by police dies in custody

Man dragged by police dies in custody
It was unclear how many officers are involved in the incident. The commander of the local police station was also suspended pending an investigation, the South African Police Service said in a statement.
The video was captured by cell phone in Daveyton, near Johannesburg, shocking the world for its brazen cruelty.
Shaky but clear, it shows a man in a red T-shirt and white sneakers talking animatedly with police officers.
The officers then handcuff him to the back of a police van, which pulls away, dragging his feet along the road. Officers and bystanders run alongside.
Some in the crowd scream as the van drives away slowly, then picks up speed.
The man, identified as a Mozambican taxi driver, died Tuesday night, a few hours after the incident, in a police cell from his head injuries, according to Amnesty International.
"We are shocked by this incident," said Moses Dlamini, a spokesman for the Police Investigative Directorate, an independent government agency that looks into possible crimes by police.
Violent crime is common in South Africa, but the incident was a harsh reminder of police brutality rampant in the nation.
The directorate received 720 new cases for investigation of suspicious deaths in custody or in other policing contexts between April 2011 and March 2012, Amnesty said.
"This appalling incident involving excessive force is the latest in an increasingly disturbing pattern of brutal police conduct in South Africa," said Noel Kututwa, Amnesty International's southern Africa director.
Police who carry out crimes do not reflect the police service as a whole, Dlamini said.
"There are many other officers who are dedicated, who uphold the law and arrest criminals all the time," he said.
Under apartheid rule in South Africa, white police officers subjected the nation's black majority to inhumane treatment. But in this case, the man and police in the video, as well as those in the crowd, are black.
Apartheid rule ended in the 1990s, and the government reformed the police departments and made them more diverse.
Despite the changes, the nation grapples with a high crime rate, including rapes, armed robberies and police brutality, analysts say.
South Africa's history of violence "is part and parcel of daily life," said Johan Burger, a senior researcher with the Institute for Security Studies in Pretoria.
Some police officers believe that they "are above the law" and that there won't be consequences for their actions, he said.
South Africa's police force has been plagued by a series of scandals recently.
In August, officers opened fire on striking platinum miners in Marikana, killing 34 in one of the most deadly police shootings since the end of apartheid.
Last month, one of its officers -- Hilton Botha -- was booted from a high-profile murder case after prosecutors reinstated attempted murder charges against him.
Botha is accused of chasing and firing on a minibus full of people while drunk in 2011. He is charged with seven counts of attempted murder.
He was testifying in the trial of Paralympic star Oscar Pistorius, who is charged with killing his girlfriend on Valentine's Day.
In the case of the taxi driver, the independent investigative agency pledged to be transparent in its findings.