Malawi Imekurupuka Kususia Mazungumzo


Katika hatua isiyotegemewa, Malawi imetangaza kujitoa katika mazungumzo ya mgogoro wa mpaka kati yake na Tanzania kwenye Ziwa Nyasa. Rais Joyce Banda wa nchi hiyo alisema mwanzoni mwa wiki aliporejea nchini mwake akitokea katika ziara ya Marekani na Uingereza kuwa, sasa mgogoro huo utapelekwa katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), kwa madai kwamba juhudi za usuluhishi wa kidiplomasia umeshindwa.


Hatua hiyo ya Rais Banda ambayo tunaweza kuiita ya kukurupuka siyo tu imeishtua Tanzania, bali pia Afrika na dunia nzima kutokana na ukweli kwamba mazungumzo kuhusu mgogoro huo yalikuwa yakiendelea vizuri chini ya usuluhishi wa jopo la marais wa zamani barani Afrika chini ya uenyekiti wa Rais mstaafu wa Msumbiji, Joachim Chissano.


Lakini waliokuwa wakifuatilia mgogoro huo kwa karibu watakubaliana nasi kwamba nchi hiyo tangu mwanzo haikuwa na dhamira ya kumaliza mgogoro huo kwa mazungumzo au usuluhishi. Mara zote zilisikika kauli na sauti za viongozi katika serikali hiyo zikibeza juhudi hizo kwamba ni kupoteza muda tu. Tangu mwanzo mkakati wa serikali hiyo ulikuwa kupeleka mgogoro huo katika mahakama za kimataifa.


Ni jambo la kushangaza Rais Banda anaposema hatua ya nchi yake kujitoa katika mazungumzo ya usuluhishi imetokana na kuhujumiwa na katibu wa jopo la usuluhishi ambaye ni raia wa Tanzania, ambaye nchi hiyo inadai alivujisha taarifa muhimu za Malawi kwa Tanzania kabla ya Tanzania haijawasilisha taarifa zake kwa jopo hilo. Kama kweli Malawi ilikuwa na ushahidi wa hujuma hizo kwa nini haikulifikisha suala hilo kwa mamlaka husika, ikiwamo kutaka hatua zichukuliwe dhidi ya katibu huyo?


Mgogoro huo wa mpaka ni wa muda mrefu na unatokana na mikataba yenye utata iliyoachwa na wakoloni. Kwa kutambua hilo marais waliotangulia, hasa Bakili Muluzi na Bingu wa Mutharika wa Malawi na wenzao Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa wa Tanzania, waliendeleza mazungumzo, kwani walitambua kwamba Ziwa Nyasa ni urithi wa wananchi wote wanaoishi katika nchi tatu za Msumbiji, Tanzania na Malawi na kwamba mazungumzo ndio suluhisho pekee la tatizo la mpaka.


Lakini kujitokeza kwa dalili za kuwapo mafuta katika Ziwa Nyasa na baadaye Rais Joyce Banda akaingia madarakani ndiko kulikosababisha Malawi isione tena umuhimu wa kuendelea na mazungumzo. Kwa maneno mengine, suala la mafuta ghafla liliichanganya na kuipofusha Serikali ya Malawi ambayo haikuona tena umuhimu wa kutoa kipaumbele kwa masuala ya ujirani mwema.


Serikali ya Rais Joyce Banda bila kushauriana na Tanzania ilitoa leseni kwa makampuni mawili ya kigeni kutafuta mafuta katika eneo la Ziwa ambalo linamilikiwa na Tanzania.
Hilo ndilo chimbuko la mgogoro uliopo hivi sasa ambao umechukua sura mpya baada ya upande mmoja wa mgogoro huo kupata ndoto za kuneemeka na mafuta.

Shilole na Q-chief Kunani? Wanaswa kwenye Mapozi Tata Ndani ya Ndege




MWANAMUZIKI wa miondoko ya mduara Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ na muimba Bongo Fleva, Abubakar Katwila ‘Q-Chillah’  hivi karibuni waliawaacha midomo wazi wasafiri ndani ya ndege kufuatia tukio lao la kufanya ‘malavidavi’ bila kujali.

Aibu hiyo ilitokea Machi 29, mwaka huu ambayo ilikuwa Ijumaa Kuu ambapo wasanii hao walikuwa wakitoka Dar kwenda Mwanza kwa ajili ya kufanya shoo siku ya Pasaka.
Akilisimulia gazeti hili, shuhuda wetu aliyekuwemo ndani ya ndege hiyo (jina tunalo) alisema aliwaona Shilole na Q-Chillah wakiwa katika ‘malovee’ ambapo mara kwa mara walikuwa wakipigana mabusu kitendo kilichowafanya abiria wengine kuwakodolea macho yenye kuwashangaa.

“Tunakubaliana na kazi zao, lakini kusema ule ukweli, sisi abiria wenzao tulishangaa sana, unajua kuonesha vitendo vya mahaba ndani ya ndege si utamaduni wetu Wabongo,” alisema abiria huyo aliyekuwa akienda Mwanza kikazi.
Aliongeza kuwa, ilifika mahali baadhi ya abiria walitaka kuwafungukia ukweli kwamba wanachokifanya si adabu hasa ikizingatiwa kuwa wao wana majina makubwa katika burudani za Bongo.
Kufuatia taarifa hizo na kudakwa kwa picha zao, Amani liliwasaka watuhumiwa hao kila mmoja kwa wakati wake ili kusikia kutoka kwao juu ya kufanya madudu ndani ya ‘pipa’.

Kwa upande wake, Shilole alisema kuwa mabusu ni vitu vya kawaida kwake ikizingatiwa Q-Chillah ni mwanamuziki mwenzake kwa hiyo hakuna tatizo.
“Jamani kwani mabusu yana shida gani, yule (Q-Chillah)  ni mwanamuziki mwenzangu na tumezoeana. Yale yalikuwa ni mambo ya kawaida tu na utani, si vinginevyo,” alisema  Shilole.
Q-Chillah simu yake ya mkononi ilikuwa ikiita muda mwingi bila kupokelewa, lakini baadhi ya watu wake wa karibu walisema mwanamuziki huyo hana kawaida ya kupokea simu kama namba hazijui. 

LAANA KANGA MOJA BUKOBA




 Hapo  wanafanya  mapenzi  live  japo  hawajavua.....Iko  haja  ya  kuwakataza  watoto  kushiriki  show  kama  hizi....kwani hazina Maadili Kabisa...

 Huyu  hata  chupi  hana.Ni  kanga  tu  tena  imefungwa  upande  mmoja.Haya  madanguro  ya  uchi  yanakera  sana...
Wewe Mdakuzi unasemaje kuhusu Style hii ya Kanga Moko ? Je kuna Ulazima Serekali kuingilia kati ?

DPP Zanzibar “Atupilia mbali uchunguzi mauwaji ya Padri Mushi




Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Zanzibar, Ibrahim Mzee Ibrahim, ametupilia mbali uchunguzi wa mauaji ya Padri Evarist Mushi uliofanywa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Maafisa wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) na kusema mtuhumiwa hana kesi ya kujibu mahakamani.

Padri Mushi ambaye alikuwa Paroko wa Kanisa Katoliki Minara Miwili aliuawa kwa kupigwa risasi Febuari 17, mwaka huu katika eneo la Beitrasi mjini hapa akiwa ndani ya gari alipokuwa akielekea kuongoza misa ya Jumapili katika Kanisa la Mtakatifu Theresia, mjini Zanzibar.

Baada ya mauaji hayo, Rais Jakaya Kikwete alitoa kibali cha kukaribisha maafisa wa FBI kushirikiana na Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa mauaji hayo na Machi 17, mwaka huu Jeshi la Polisi lilimkamata Omar Mussa Makame kwa tuhuma za kuhusika na mauaji hayo.

Uchunguzi wa NIPASHE umebaini kuwa DPP baada ya kulipitia jalada la uchunguzi wa mauaji hayo, juzi alitoa mwongozo kwa Jeshi la Polisi kuendelea kumtafuta muuaji wa Padri Mushi.

Kwa mujibu wa uchunguzi huo, DPP aliliandikia barua Jeshi la Polisi na kukabidhiwa juzi ikieleza sababu za ofisi yake kutofungua hati ya mashtaka hadi sasa dhidi ya mtuhumiwa wa mauaji hayo.

Jeshi la Polisi limethibitisha kuipokea barua ya DPP ambayo inaeleza kuwa ushahidi uliokusanywa katika jalada la kesi hiyo hauna mashiko na kwamba mtuhumiwa hahusiki na mauaji hayo.

Chanzo cha habari kutoka Jeshi la Polisi kilieleza kuwa DPP hajaridhishwa na uchunguzi wote uliokusanywa dhidi ya mtuhumiwa pamoja na watuhumiwa watatu wanaotuhumiwa kwa mauaji ya askari polisi, Said Abdulrahman aliyeuawa kwa kupigwa mapanga na watu wanaosadikiwa kuwa wafuasi wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar Oktoba 17, mwaka jana.

Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa, alithibitisha hatua ya DPP kutupa uchunguzi wote wa jalada la mauaji ya Padri Mushi na kuwataka waandishi wa habari kumtafuta DPP azungumzie sababu za uamuzi wake wa kutokubaliana na uchunguzi wa Polisi.

Hata hivyo, alisema kwamba Jeshi la Polisi bado linaamini uchunguzi walioufanya kwa kushirikiana na FBI hauna shaka na kwamba mtuhumiwa huyo ana kesi ya kujibu mahakamani na wataendelea kumshikilia.

Alisema kwamba kwa mujibu wa sheria, Jeshi la Polisi jukumu lake ni kuchunguza kesi na ofisi ya DPP jukumu lake ni kufungua hati ya mashtaka na kutetea kesi mahakamani.

Hata hivyo, NIPASHE ilipofika katika ofisi ya DPP, Katibu muhtasi wake alisema amepokea maagizo kutoka kwa bosi wake kuwa waandishi wote wa habari wanaofuatilia suala hilo, wamuone Kamishna wa Polisi kwa vile kazi aliyopewa ya kupitia jalada la uchunguzi kabla ya kufungua kesi ameikamilisha.

“Kamishna ndiye aliyeitisha mkutano na waandishi wa habari kuelezea hatua iliyofikiwa pamoja na kukamatwa kwa mtuhumiwa, sasa awaite tena amalizie kazi yake ya kuwaeleza hatua iliyofikiwa baada ya Mkurugenzi kurejesha jalada la mauaji,” alisema Katibu muhtasi huyo.

Katika hatua nyingine, Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai, Yusuph Ilembo, jana alifika katika Mahakama Kuu ya Zanzibar, kufuatia ombi lililofunguliwa mahakamani na wakili anayemtetea mtuhumiwa wa mauaji, Abdallah Juma Mohamed.

Abdallah Juma amefungua ombi katika Mahakama Kuu kwa kutumia kifungu cha sheria 390 cha sheria namba 7 ya mwenendo wa makosa ya jinai ya mwaka 2004, akitaka Jeshi la Polisi litoe maelezo kwa nini mteja wake hajafikishwa mahakamani ndani ya saa 24 tangu alipokamatwa Machi 17, mwaka huu.

Wakili Abdallah Juma akisaidiwa na mawakili Shaban Juma Bakari na Shaibu Ibrahim Shaibu waliitaka Mahakama Kuu itoe amri ya kuachiwa kwa mteja wao kutoka mikononi mwa Jeshi la Polisi. Hata hivyo, Ilembo alisema kuwa kutokana na uzito wa kesi hiyo, anaomba kupewa muda wa kutayarisha majibu ya hati ya kiapo kwa maandishi na kuuwasilisha kwa upande wa utetezi na mbele ya mahakama hiyo kabla ya ombi hilo kuanza kusikilizwa na kutolewa uamuzi.

“Tunaomba mtuhumiwa aendelee kushikiliwa na Polisi, wakati tukifanya matayarisho ya kujibu hati ya kiapo,” alisema Ilembo.

Kwa upande wake Jaji wa Mahakama Kuu, Mkusa Isaack Sepetu, alisema baada ya kusikiliza pande zote mbili, alimtaka Ilembo awe amejibu kwa maandishi hati ya kiapo ya maombi hayo kabla ya kuanza kusikilizwa kwa shauri hilo Aprili 8, mwaka huu.

Aidha, Jaji alisema wakati wa kusikilizwa kwa shauri hilo, ametaka mtuhumiwa huyo afikishwe mahakamani, baada ya hoja za upande wa mawakili wanaomtetea kutaka dhamana kwa mteja wao, kwa vile bado hajafikishwa mahakamani kwa tuhuma za mauaji.

Kutupwa kwa uchunguzi wa jalada la mauaji hayo pamoja na jalada la uchunguzi wa mauaji ya Polisi kunadhihirisha kuwapo kwa mvutano mkubwa baina ya Jeshi la Polisi Zanzibar na ofisi ya DPP.

CHANZO: NIPASHE

PICHA ZA MATUKIO YA VURUGU HUKO TUNDUMA......DIWANI ( CHADEMA ) NA MCHUNGAJI WA KKKT WANASAKWA NA POLISI



Hii ndiyo hali halisi ya Mji mdogo wa Tunduma leo kuanzia asubuhi

Matairi yanachomwa katikati ya barabara

Mambo hayo 



Mwandishi wetu pamoja na waandishi wenzake walipata shida sana kufika mji wa Tunduma walikutana na vikwazo vingi sana lakini wananchi walikuwa waelewa waliwasaidia kutoa magogo na matairi ili wapite wakapate habari












Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Diwani akiongea na waandishi wa habari
Wanafunzi wakisindikizwa na jeshi la polisi kurudi majumbani mwao
Polisi wakiendelea na kazi yao katika mitaa ya Tunduma
Baadhi ya magari ya IT yaendayo nchini Zambia yakiwa yamepakiwa nnje kidogo ya mji wa Tunduma kuogopa kuharibiwa kwa magari hayo

----------------
Diwani wa kata ya Tunduma Ndugu Frank Mwaijoka (Chadema) pamoja na mchungaji wa kanisa la KKT katika eneo hilo la Tunduma wilayani momba Mkoani mbeya wametakiwa kujisalimisha kituo cha Polisi Tunduma mara baada ya kuhusika na uchochezi wa kidini hali ambayo imepelekea kutokea kwa vurugu  katika eneo hilo.

Vurugu hizo zimeanza majira ya saa 4 asubuhi katika eneo hilo la tunduma mara baada ya kundi la watu wanaodai kuwa wao ni wafuasi wa dini ya kikristo wakidai waruhusiwe kuchinja mifugo na kuuza katika mabucha yao hali iliyo pelekea kuibuka kwa vurugu hizo.

Akizungumza kuhusiana na tukio hilko Kamanda wa Polisi Mkoani humo Ndugu Diwani Athumani amesema kuwa kufuatia kuwepo kwa tukio hilo jumla ya watu zaidi ya 40 tayari wamekwisha kamatwa .

Amesema mpaka sasa taarifa walizo zipata kufuatia vurugu hizo zinaeleza kuwa miongoni mwa watu walichochea vurugu hizo ni diwani wa kata hiyo ya Tunduma Ndugu John Mwaijoka pamoja na Mchungaji wa kanisa la kkt ndugu Neema Mwaipusa ambao kwa pamoja wametakiwa kujisalimisha kituo cha polisi kwa mahojiano zaidi.

Amesema suala hilo limegubikwa  na siasa kwani tayari viongozi wa serikali akiwemo Mkuu wa mkoa huo Ndugu Abbas Kandoro amekwisha litolea ufafanuzi Apri 02 mwaka huu wakiwepo pia viongozi wa dini .
Amesema kwa asilimia kubwa mgogoro huo juu ya nani achinje umeingiliwa na mambo ya kisiasa kwani hata baadhi ya wananchi wa maeneo hayo wamekuwa wakilalamika juu ya kutokea kwa vurugu hizo.

Amesema shughuli za kibiashara katika eneo hilo zimeshindwa kufanyika katika eneo hilo hivyo kufanya wananchi kupata adha hasa kwa nchi jirani ya Zambia ambao kwa asilimia kubwa wanategema kupata mahitaji kutoka mpakani mwa Tanzania.

Hata hivyo Diwani amesema kuwa katika vurugu hizo askari mmoja  pamoja na mwananchi wamejeruhiwa kwa kupigwa mawe ambapo tayari wamekwisha fikishwa kituo cha polisi.

Kufuatia hali hiyo Kamanda huyo wa Polisi amesema kwa sasa hali imelejea katika hali yake ya kawaida hivyo amewataka wananchi wa maeneo hayo kuwa watulivu wakati jeshi hilo la Polisi likiendela na msako wa kuwatafuta wahalifu wengine.

RIPOTI MAALUMU KUHUSU VURUGU ZA TUNDUMA ZILIZOSABABISHA MIPAKA KUFUNGWA KWA MUDA



Taarifa  kutoka Tunduma mkoani Mbeya zinadai  kuwa hali  si shwari katika eneo hilo kutokana na kuzuka kwa  vurugu kubwa zinazodaiwa kusababishwa na masuala ya  kiimani ya nani achinje kati ya mkristo na Muislam .

Mwandishi   wetu  kutoka Tunduma mkoani Mbeya  anaripoti kuwa  vurugu  hizo zimeanza  majira ya saa nne asubuhi  kwa makundi  ya vijana  kuandamana mitaani na kuvutana  kuhusu uamuzi  wa viongozi  wa dini ya kikristo Tunduma  kuandika barua kwa mkuu  wa wilaya  kutaka  kuruhusiwa kuchinja  wakati wa pasaka.

Ripota  wetu anaripoti   kuwa kabla ya  ijumaa kuu  viongozi hao  wa dini ya Kikristo  walikutana na mkuu  wa  wilaya  ya Momba Abuud Saibea ambae  aliwataka kuwasilisha barua rasmi ya  kutaka  kibali  cha  kuchinja .

Hata hivyo inaelezwa  kuwa  vurugu  hizo za  leo zina mikanganyiko  mingi  kwani  wanaoshiriki katika  vurugu  hizo ni vijana  wapiga debe .....

Vurugu za  uchinjaji  zilifanyika  siku ya Pasaka  na hazikuwa na mvutano  kwa sababu wakristo  walichinja katika bucha zao na  waislamu nao  walichinja katika mabucha yao ....

Cha kushangaza leo ni baada ya  kuibuka  kundi  la  vijana  wanaofanya kazi katika stendi na vijiwe mbali mbali ambao  ndio walioanzisha  vurugu kiasi cha  polisi  kuingilia kati kwa kutumia mabomu ya machozi na kuwatawanya  wananchi  waliokuwa wamekusanyika maeneo mbali mbali .

Kutokana na vurugu  hizo mpaka  wa Tunduma  ambao unaingia nchi  za kusini  mwa Tanzania  ulifungwa  pamoja na magari yaliyokuwa yakitoka  Sumbawanga  pia  yalizuiwa  kuendelea na  safari hadi hali  hiyo  ilipotulia mida ya saa 8 mchana baada ya kamanda wa polisi wa mkoa  wa Mbeya  Diwani Athuman  kufika  eneo hilo.


BREAKING NEWS: HALI NI MBAYA HUKO TUNDUMA....MABOMU KILA MAHALI NA WATU WAMEAMRIWA WASITOKE NJE


Masaa takribani matano mabomu ya machozi na risasi za moto zinasikika mataili yamechomwa barabarani maduka yote yamefungwa...
 Ni mshikemshike kati ya vyombo vya dola na raia hadi sasa msikiti mmoja umechomwa moto maeneo ya mwaka na kisimani  
Hali ni mbaya zaidi kwan mabomu ya mochozi yanapigwa hadi vyumbani. 
Imetollewa amri watu wote walale majumbani kwao
Chanzo  cha  tatizo  ni  waislam  na  wakristo.Wametofautiana  juu  ya  swala  la  kuchinja.

STAY TUNED: MORE NEWS TO COME