
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, ambae pia ni Mbunge wa Hai na kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzania Bungeni Mh Freeman Mbowe akizungumza na waandishi wa habari jana jioni katika uwanja wa hospitali ya Mt Meru mara baada ya kutembelea kuwapa pole majeruhi wote waliolazwa katika hospitali hiyo kutokana na majeraha ya yaliyosababishwa na mlipuko wa bomu la kurushwa kwa mkono katika kanisa la Mt Joseph Mfanyakazi-Olasiti lililotokea jumapili iliypoita.
Katika mazungumzo yake Mh Mbowe aliwapa pole wote waliofikwa na janga hilo na kuwataka watanzania wote wawe watulivu huku vyombo vya dola vikifanya kazi yake lengo likiwa ni kuwapata wahusika na ijulikane hasa lengo lao kulipua bomu kanisani lilikuwa ni nini. Baada ya kutoka hopsitalini hapo Mbowe na msafara wake walielekea Elerai kuhani msiba mmojawapo.

Waumini wa Kikatoliki wakimsikiliza Mh Mbowe (haonekani pichani) wakati alipofika kanisani hapo kuwapa pole.

Mh Mbowe akihutubia waumini wa Kanisa Katoliki Mt Joseph – Olasiti jana. Aliyemshikia kipaza sauti ni Mbunge wa Arumeru Mashariki, Mh Joshua Nassari.

Mb Mbowe akipatiwa maelekezo namna siku ya shambulio hali ilivyokuwa na Padri Festus Mangwangi wa Kanisa la Mt Josephat Mfanyakazi.Olasiti Arusha

Mh Mbowe akiwa ndani ya kanisa hilo

Padri Festus Mangwangi akielekeza mahali bomu lilipoangukia na namna watuwalivyojiokoa. Mbowe katika msafara wake aliambatana na wabunge wa chama hicho kwa majimbo ya Arusha Mjini na Arumeru Mashariki, pamoja na viongozi wa juu wa chama na Kanda ya Kaskazini.

Mh Mbowe akiondoka eneo la kanisa mara baada ya kuzungumza na mapadri na waumini

Mbowe na viongozi wengine wa chama na wabunge wakisubiri kuruhusiwa kuingia eneo la kansia ambalo muda huo kulikuwa na ulinzi mkali kusubiri ujio wa Rais Kikwete

Wafuasi na viongozi wa Chadema Arusha wakimsubiria Mwenyekiti wao Mbowe katika geti la wanaowasili uwanja mdogo wa ndege Arusha.

Mbowe akiwasili uwanja mdogo wa ndege Arusha mchana wa jana na kulakiwa na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, Mbunge wa Arumeru Mashariki, Mh Joshua Nassari, Katibu wa Chadema Arusha na Kanda ya Kaskazini, Mh Amani Golugwa na Mwenyekiti wa Chadema Arusha Mh Samson Mwigamba.

Chritopher Mbajo, wa Chadema Same anayefanya shughjuli zake Arusha akimtambulisha Mh Mbowe kwa makamanda waliokusanyika nje ya uwanja mdogo wa ndege Arusha kwa ajili ya kumpokea

Mh Mbowe akimjulia hali Apolinary Malamsha aliyelazwa hospitali ya St Elizabeth. Hospitali hiyo ina majeruhi 20 na baadhi yao bado wana vyuma vya bomu mwilini.

Mbowe akizungumza na daktari wa hospitali ya St Elizabeth ya jijini Arusha

Mbowe akimjulia hali mtoto aliyejeruhiwa na bomu na kulazwa hospitali ya Mt Meru.

Mbowe akimfariji majeruhi Samwel Pius aliyelazwa hospitali ya St Elizabeth

Mjeruhi mwingine hopitali ya Mt Meru

Mh Mbowe akisalimiana na wauguzi wa hospitali ya St Elizabeth

Mh Mbowe akisaini kitabu cha wageni hospitali ya St Elizabeth

Mh Mbowe katika ukumbi wa VIP uwanja mdogo wa ndege Arusha

Mh Mbowe akizongwa na kina mama waliokuwa na shuku ya kumshika tu mkono alipozuru hopitali ya Mt Meru

Kamanda wa Chadema Jijini Arusha maarufu kama Omar Matelephone akiwa na wenzake uwanja wa ndege Arusha. Mh Mbowe alipokelewa na msafara wa magari 30 chini ya usimamizi wa Omary na mtu mwingine aliyetambulishwa kama Magoma Derick Magoma

Mh Mbowe na viongozi wa chama (CHADEMA) katika ofisi ya chama hicho