LUSHOTO YAGEUKA UWANJA WA VITA BAADA YA RISASI ZA MOTO KURINDIMA ANGANI

Wilaya ya Lushoto Katika jimbo la Mlalo jana
kuligeuka uwanja wa vita ama baada ya Makada wa ccm kufyatua Risasi hewani mfulululizo kuwatisha weananchi ambao walikuwa maeneo ya Mnadani hapo lukozi....


Katika tukio hili Viongozi wa Chadema wanajipanga kulipoti police leo Asubuhi.

Tukio lilikuwa kama hivi:


 Makada wa ccm wakiongozwa na kamanda wa vijana wilaya ccm Nasri , mtoto wa Mzee mndolwa faustine walikuwa wakizima upepo wa ushindi wa Chadema iliyoupata hivi karibuni kwa kushinda vijiji vitano 5 kwa mara ya kwanza katika historia ya vyama vingi kuingia nchi. 

Ccm wakiwa kwenye mikutano yao walikuwa maeneo ya lukozi ndipo Wananchi walipo wahoji kwa sera zao mbaya na zisizo na matumaini kwa kuwaambia hawaitaji tena na wananchi wanawataka waondoke ...


Wanachi hao waliokuwa kwenye mkusanyiko huo walipaza sauti zao kwa kusema wanawaomba waondoke huku wakiwazomea ndipo makada hao  walipo amua kulipua Risasi hewani