WAMERU WACHARUKA! WAMFUHATA MBUNGE WAO NASSARI NA KUSEMA WATAMLINDA WENYEWE


WAZUNGUKA NA MAJANI MJI MZIMA NA KUZINGIRA HOSPITALI YA SELIAN.

WASHANGA KWANINI WALIO HUSIKA AWAJA KAMATAWA?

WAIZINGILA HOSPITALI NA KUONYA KITAKACHO MPATA MBUNGE WAO WENYEWE WATAJIBU.

HOFU YATANDA WANAUSALAMA WASHAULI NASSARI AHAMISHIWE.

KUNAUVUMI KUWA MABOMBA YA KUPELEKA MAJI MONDOLI YAKATWA.


Hawa ni baadhi ya wameru walio handamana kutoka Meru wakielekea Hospitali yaSeliani Jana


Joshua Nassari akiongea na waziri mkuu alipokuja mtembelea Hospitali jana.


wananchi wakiwa kwenye uzio wa hospitali ya Seliani wakiimba na kumdai mbunge wao ili waondoke nae.





UPDATES FROM SOWETO ARUSHA

Askari Polisi kwa wingi wao, wakiwa na mabomu ya machozi, bunduki za risasi, maji ya kuwasha n.k, wamedamkia viwanja vya Soweto na kuweka zuio mtu yeyote asiingie ndani ya eneo hilo ambalo tayari kuna mahema na viti kwa ajili ya wanaChadema na watu wengine kuweza kushiriki tukio la kuaga marehemu waliokufa kwenye mlipuko wa bomu ambalo Mh Mbowe alitangaza jana kuwa mrushaji ni askari Polisi na watamtaja muda wowote wakimaliza kushauriana na wanasheria wa chama.
Kwa makadirio ya haraka mpaka sasa kuna watu kati ya 600 na 700 wameshatanda eneo hilo wakiwashangaa Polisi hao na zoezi linaloendelea wakidai hakuna kibali cha mkusanyiko eneo hilo. 

Haya ni maajabu mengine na ni sababu ya kuongeza tension kwa watu wenye majonzi... Kuna taarifa pia Askari wa JWTZ hawajapendezwa na hatua hiyo na wameshangaa ni kwanini watu wanazuiwa ilhali na viongozi wao wako hapo kuaga wapendwa wao. 

Ikumbukwe kwamba jana mtoto meingine ameongezeka kwenye idadi ya waliofariki na kuna watu kadaa wako ICU Arusha na Nairobi ambao sala zenu na dua zenu zitawaponya. 

Mmoja wa walioko ICU ya Selian Hospital ni pamoja na Meneja Kampeni wa Mgombea wa Chadema Kata ya Elerai ambae kwasasa hawezi kuongea tena. Anafahamika kama Bw Gabo. Gabo ana mtoto wa miaka miwili na marehemu Judy Mollel, Katibu wa Chadema Sokoni 1 na aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Bawacha katika Kata hiyo..Judy alifariki papo hapo baada ya kulipiliwa na bomu akiwa na mwenza wake huyo ambao wote ni viongozi wa Chadema Arusha. 
Inatia simanzi na kuhuzunisha sana, na hasira pia (Mbowe aliwaambia maelfu ya wananchi jana walilipize kwa chochote zaidi ya sala kwa Mungu) hasa ukizingatia kuwa wahusika ni askari polisi na leo wanawazuia watu wasiage wapendwa wao!! So painful. 
Ushauri wangu, kama vipi hili Jeshi la Polisi na waliowatuma wazichukue maiti hizo wakazichemshe supu wanyewe ikiwa hawaguswi na chochoite katika hili. Ifahamike kuwa sio askari wote wakubwa kwa wadogo wamependezwa na yaliyaofanyika lakini kitendo cha kuweka vizuizi hivi kunawajumuisha wote na Jeshi zima. Kikubwa walipaswa kuonesha ushirikiano na kuongeza ulinzi kwa wale walio wema kwasababu hata jana Mbowe aliwataka wananchi kuacha hasira zao na wasiwazuie Polisi kufanya kazi zao. 


Ni hayo kwa sasa (picha iliyotumika ni ya mkusanyiko wa jana viwanja vya Soweto ambapo Mbowe alitoa taarifa zaidi kuhusiana na sakata hilo na kuweka bayana kuwa mhusika wamenfahamu kupitia rekodi za video viwanjani hapo) 

SeriaMtoto WikiLiks Tumainiel ON FB

CHADEMA:MLIPUAJI WA BOMU NI POLICE: HATUKUBALI MAUAJI YA AINA HII

MBOWE:BOMU LILIRUSHWA NA FFU NA USHAHIDI UPO


MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe amefichua siri kuhusu tukio la mlipuko wa bomu lililotokea jusi katika viwanja vya Soweto, jijini Arusha.

Katika kauli yake jana, Mbowe ameibua tuhuma nzito dhidi ya Jeshi la Polisi, ambapo alidai kuwa askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) ndiye aliyerusha bomu hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa,baada ya kutembelea majeruhi katika Hospitali ya Selian, Mbowe alisema chama chake kina ushahidi wa kutosha juu ya askari huyo kurusha bomu.

Mbowe ambaye pia ni kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni,alisema wamefanikiwa kupata ushahidi wa kutosha juu ya tukio hilo baya linalochafua taswira ya nchi.

Alisema chama chake kipo tayari kuweka ushahidi huo hadharani, iwapo Serikali itaendelea kufanya siasa na kuficha ukweli. 

“Tunao ushahidi wa kutosha, ikiwamo wa picha za video unaoonyesha shambulio la bomu na risasi lilivyofanyika katika mkutano wangu jusi eneo la Soweto.

“Picha zinaonesha wazi aina ya silaha zilizotumika kwenye shambulio lile ni tatu, bomu la gurumeti ambalo lilitupwa na askari wa FFU aliyekuwa kwenye uniform.

“Kutokana na ushahidi huu tulikuwa tumewaeleza Polisi kama wataendelea kuficha tutaueleza umma na tutaiambia dunia, kwani aina ya silaha zilizotumika ni SMG na bastola.

“Makasha ya risasi kama ushahidi wa jambo hili zilizotumika tuliyaokota eneo la tukio na tayari tumeyarekodi na kuyakabidhi kwa askari waliokuwa wakichunguza tukio lile,” alisema Mbowe.

Hata hivyo Mbowe alipinga tamko la Serikali kupitia Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uratibu na Bunge), William Lukuvi na kusema kauli yake ni ya kitoto mbele ya jamii.

“Kauli ya Serikali kupitia kwa Lukuvi kwamba vurugu zilisababishwa na vikundi, wanasiasa na mashirika yasiyo ya kiserikali ambavyo havijulikani ni sawa na kuwadhihaki Watanzania,” alisema.

Kutokana na hali hiyo Mbowe alisema tayari wanasheria wa chama hicho akiwemo Mabere Marando, Tundu Lissu na Profesa Abdallah Safari wanashughulikia suala hilo.

Alisema baada ya polisi huyo kurusha bomu, alikimbilia katika gari ya Toyota Land Cruizer yenye rangi ya bluu akiongozana na askari mwenzake ambapo gari hilo liliondoka kwa kasi, huku likisindikizwa kwa kukingwa na gari ya TDI hadi kituo cha polisi.

Mtanzania

White House cancels Obama safari in Tanzania: report


US President Barack Obama and First Lady Michelle Obama wave to supporters after delivering remarks during a campaign event in Davenport, Iowa. The White House has cancelled a safari that President Obama and Michelle were due to take in Tanzania over budgetary concerns, The Washington Post reported June 13, 2013. FILEWASHINGTON




The WhiteHouse has cancelled a safari that US President Barack Obama and his wife Michelle were due to take in Tanzania over budgetary concerns, The Washington Post reported Thursday.


The newspaper, citing a Secret Service planning document, said the excursion scheduled during a tour of Africa that Obama will undertake later this month would have required agents protecting him to take extraordinary precautions.


IN SUMMARY

The excursion would have required agents protecting him to take extraordinary precautions. 
A trip to South Africa's Robben Island, the site of the prison where anti-apartheid hero Nelson Mandela was held, had taken precedence. 
Hundreds of Secret Service agents will be dispatched for the president's visit. 
A Navy aircraft carrier or amphibious ship with a fully staffed medical trauma centre will be stationed offshore. 
Dozens of vehicles will also be brought to the three countries by military transport planes, along with sheets of bulletproof glass to cover the windows of the hotels where the Obamas stay. 


The safari "would have required the president's special counterassault team to carry sniper rifles with high-calibre rounds that could neutralise cheetahs, lions or other animals if they became a threat," the paper reported.


Outlining the vast security preparations made for Obama's trip to Senegal, Tanzania and South Africa, the document was provided to the Post by a person "concerned about the amount of resources necessary for the trip." It did not provide cost information.


The Post said the WhiteHouse cancelled the safari Wednesday after the paper inquired about the "purpose and expense." The Obamas had been expected to spend more than two hours at Tanzania's Mikumi National Park. The WhiteHouse was not immediately available for comment, but a spokesman told the Post that a trip to South Africa's Robben Island, the site of the prison where anti-apartheid hero Nelson Mandela was held, had taken precedence.


"We do not have a limitless supply of assets to support presidential missions, and we prioritised a visit to Robben Island over a two-hour safari in Tanzania," said the spokesman, Josh Earnest. "Unfortunately, we couldn't do both." The Post said Obama's Africa tour, his first since taking office in January 2009, could cost the government between $60 million and $100 million, based on cost of similar trips in recent years.


The report comes as many government agencies struggle with mandatory budget cuts that took effect in March because US lawmakers failed to strike a wider budget deal. Hundreds of Secret Service agents will be dispatched for the president's visit, along with a Navy aircraft carrier or amphibious ship, with a fully staffed medical trauma centre stationed offshore, the report said.


Dozens of vehicles will also be brought to the three countries by military transport planes, along with sheets of bulletproof glass to cover the windows of the hotels where the Obamas stay. "Fighter jets will fly in shifts, giving 24-hour coverage over the president's airspace," the report said, citing the Secret Service document.


NAPE NNAUYE: TUKIO LA BOMU ARUSHA LILIPANGWA NA CHADEMA:ISOME TAARIFA YAKE HAPA.



Itakumbukwa tarehe 16/06/2013 ilikuwa ni siku ya uchaguzi mdogo wa madiwani kwa baadhi ya kata nchini. Uchaguzi huo umefanyika kwenye kata ishirini na mbili (22) -kati ya kata ishirini na sita (26) zilizotangazwa kufanya uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi wazi.

Matokeo tuliyoyapata toka kwenye maeneo yaliyofanya uchaguzi yanaonyesha kuwa kati ya kata 22 zilizofanya uchaguzi CCM tumeshinda kata 16 sawa na asilimia 72.72% na wenzetu wamechukua kata 6 zilizobaki sawa na asilimia 27.28%.

Tunawashukuru sana kote walikoonyesha imani yao kubwa kwa Chama chetu kwa kutupa dhamana ya kuendelea kuwatumikia. CCM inawaahidi utumishi uliotukuka.


Hata wale 27.28% walioamua kuwajaribu wenzetu, tunawatakia kila lakheri, kwani wametumia haki yao ya kidemokrasia kuchagua wanaodhani watawasaidia kufikia malengo yao ya kimaendeleo. Uchaguzi kwenye kata hizi zote umeisha sasa tuwatumikie wananchi.

Kata nne za jiji la Arusha hazikufanya uchaguzi baada ya kuahirishwa kufuatia tukio la kusikitisha la kulipuka kwa bomu kwenye mkutano wa kampeni wa Chadema mjini Arusha tarehe 15/06/2013.

CCM tunalaani tukio hilo la mlipuko wa bomu na matukio yanayofanana na hayo katika nchi yetu. Tunawapa pole wale wote walioathirika na tukio hilo. 

Ni vizuri serikali ikalichunguza swala hili kwa kutumia muda mfupi na kuhakikisha waliohusika wanapatikana na kuchukuliwa hatua zinazostahili.

Pamoja na kulaani na kuitaka serikali kukomesha vitendo hivi nchini, ni wakati muafaka kwa vyama vya siasa nchini kujitazama upya kwanikuna kila dalili kuwa tukio hili kama alivyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari mhe. Mbowe Mwenyekiti wa Chadema Taifa kuwa ni la kupangwa, inawezekana limepangwa na Chadema wenyewe.

Hali ya kisiasa jijini Arusha kuelekea uchaguzi huo ilikuwa wazi kuwa wana Arusha walishaamua kuzirudisha kata hizo nne kwa CCM, hasa baada ya kuchoshwa na maandamano na vurugu za kila siku jijini Arusha. 

Aidha kauli za kukata tamaa za viongozi wa Chadema na vitendo vyao ni dalili tosha kuwa tukio hili lilipangwa na Chadema wenyewe.

CCM tunaendelea kusisitiza na kulaani juhudi za wenzetu kujaribu kujenga umaarufu wa chama chao juu ya damu za Watanzania. Juhudi hizi zinapaswa kulaaniwa na wazalendo wote ndani na nje ya nchi.


Tukumbuke asiyekubali kushindwa, si mshindani. Si busara wala uungwana na ni kinyume na utu kutumia majanga ya kutengeneza kama mtaji wa kisiasa.

Lakini CCM tunalaani pia kitendo cha viongozi wa Chadema kujaribu kutumia baadhi ya misiba na majeruhi wa tukio hili kisiasa na mwisho wa siku kwenda kuwatelekeza hospitali baadhi yao baada ya kuwaahidi kubeba gharama zote za matibabu na mazishi.

Tunaipongeza serikali kwa kuingilia kati na kuwasaidia waathirika hawa na kuhakikisha wanapata huduma inayostahili.

CCM inarudia kueleza masikitiko yake kwa waathirika wa tukio hili la kinyama na kikatili lisilostahili kuvumiliwa hata kidogo. 

Kama Chama tumeguswa sana na tukio hili pamoja na kulilaani, tunawasihi watanzania tushindane na kutofautiana bila kupigana na kuvunja tunu ya nchi yetu ya amani na utulivu. 

Katika demokrasia ya vyama vingi swala la kuvumiliana ni swala la msingi sana katika kufikia ukomavu wa demokrasia hiyo.

Imetolewa;
Nape Moses Nnauye
Katibu wa CCM Itikadi na Uenezi.
17/06/2013

MBOWE:Hata kama utaamua Mbowe au (Godbless) Lema, huwezi kuiua CHADEMA wanachama wengine wataendeleza harakati za chama kama kawaida,




MWENYEKITI wa CHADEMA Freeman Mbowe, amevituhumu vyombo vya dola kuwa vinawafahamu watu walioshiriki kwenye mlipuko wa bomu uliotokea juzi katika viwanja vya Soweto kwenye mkutano wa chama hicho.

Mbowe, alisema tukio hilo ni la kupangwa na wamegundua risasi za bunduki aina ya SMG na bastola zilitumika mara baada ya mlipuko huo jambo linalozusha hofu na kudidimiza demokrasia ya vyama vingi.

Wakati Mbowe akitoa tuhuma hizo kwa vyombo vya dola, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema ameunda timu itakayoongozwa na makamishna wawili (Paul Chagonja na Isaya Mungulu), kwenda mkoani Arusha kuongeza nguvu ya uchunguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana mkoani hapa, Mbowe alisema uchunguzi wa awali walioufanya wamebaini tukio hilo ni la kisiasa na lilipangwa.

Alisema ni vema serikali ikatangaza kuachana na mfumo wa vyama vingi kuliko kuruhusu mauaji na vurugu katika mikutano ya vyama vya upinzani vinavyoonekana kutoa wakati mgumu kwa watawala.

Aliongeza kuwa uchunguzi wa awali katika eneo la tukio umebaini bomu lililolipuliwa ni la kiwandani na si la kutengenezwa.

Alisema katika eneo la tukio maganda ya risasi kutoka katika bunduki ya SMG na bastola yalikutwa hali inayowafanya waamini kuna watu waliamua kufanya tukio hilo kwa kupanga.

Mbowe alisema risasi hizo pia ni miongoni mwa zilizopigwa kwenye tanki la mafuta la gari la matangazo la CHADEMA ambapo zililitoboa.

Alibainisha kuwa inavyoonekana wahusika walitaka kuzalisha mlipuko mwingine mkubwa na kuleta maafa makubwa katika mkutano huo.

“Haihitaji uchunguzi wa kwenda mwezini katika suala hili, ni wazi walipanga kutuua lakini wakaua watu wasiohusika. Waliouawa hawakuwa katika mpango wao na wamekuwa wahanga kwa niaba yetu.

“Hata kama utaamua kumuua Mbowe au (Godbless) Lema, huwezi kuiua CHADEMA kwani chama kitabaki, na wanachama wengine wataendeleza harakati za chama kama kawaida,” alisema.

Wabunge kutohudhuria Bunge

Mbowe alisema kutokana na tukio hilo ambalo limeua watu zaidi ya watatu, CHADEMA imeamua kulifanya ni la kitaifa na wabunge wake watashiriki kwenye maombolezo.

Alisema kuanzia leo wabunge wote wa CHADEMA hawatahudhuria vikao vya Bunge na watajumuika mkoani Arusha hadi misiba yote itakapomalizika.

Alisema wanatarajia kufunga mahema katika eneo la tukio na marehemu wote wataagwa katika eneo hilo ambapo ibada zote za Kiislamu na Kikristu zitafanyikia hapo.

IGP aunda timu

Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Mwema ameunda timu ya kuongeza nguvu ya uchunguzi itakayoongozwa na makamishna wawili ambao ni Paul Chagonja kutoka idara ya operesheni na Isaya Mngulu kutoka ofisi ya upelelezi makao makuu.

IGP Mwema alisema baada ya tukio hilo, jeshi hilo lilituma makamishna wawili kutoka makao makuu kwa ajili ya kuongeza nguvu ya uchunguzi wa tukio hilo na kwamba wameshaanza kukusanya taarifa mbalimbali zitakazoweza kusaidia kuwabaini watu waliohusika.

Alisema wameunganisha nguvu na vyombo vingine vya ulinzi na watawasaka wahalifu hao pamoja na walio nyuma yao kwa kile alichoeleza tukio hilo linaashiria kushamiri kwa matendo ya kigaidi nchini.

Akizungumzia tuhuma zinazotolewa na wananchi juu ya Jeshi la Polisi kuwajeruhi watu kwa risasi za moto, IGP Mwema alisema kila taarifa inafanyiwa kazi kwa umakini na kwamba baada ya uchunguzi watatoa taarifa kamili kwa umma juu ya kilichotokea jijini Arusha.

Aliwaomba wananchi wenye taarifa za kuweza kumtambua aliyerusha bomu pamoja na watu walio nyuma yake wajitokeze au wamtumie ujumbe kupitia simu yake ya mkononi namba 0754 78 55 57 na kwamba uhusika wao utafanywa kuwa siri.

IGP Mwema pia alisema watachunguza kauli ya Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) bara, Mwigulu Nchemba aliyowaambia wakazi wa Kimandolu kuwa wasipoichagua CCM katika uchaguzi wa madiwani wa Jiji la Arusha ulioahirishwa jana, watakufa.

Mwema alisema watachunguza kauli hiyo baada ya kuulizwa swali la hatua zilichochukuliwa kabla na baada ya mlipuko huo dhidi ya kauli ya Nchemba.

Juzi katika mkutano wa kufunga kampeni za udiwani kwa CHADEMA uliofanyika kwenye viwanja vya Soweto, kitu kinachodhaniwa ni bomu kilipuka na kuua watu watatu na wengine kujeruhiwa.

MBOWE ATEMBELEA ENEO LA MLIPUKO, PAMOJA NA KUTEMBELEA FAMILIA ZA WAFIWA NA MAJERUHI WA MABOMU NA RISASI ARUSHA


Mwenyekiti wa Chadema, Mh freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini Mh Godbless Lema wakiwa katika uwanja wa Soweto mchana wa leo wakati zoezi la kuchukua vipimo mbalimbali likiendelea chini ya usimamizi wa wataalamu toka Jeshini.

Mbowe na Lema wakishauriana jambo..
Eneo la maafa. Inaelezwa kuwa wataalamu wa jeshi waligundua kuwako kwa kitu ndani ya tanki la mafuta na hivyo kuamua kulikata. Taarifa hizo zinadai kwamba kulikuwa na mabomu yametegwa chini ya gari na hivyo tank hilo lilishmabuliwa kwa risasi labda utokee mlipuko! Pia gari hii ya amatangazo ina majeraha mawili mlango wa kushoto yaliyotokana na kitu chenye ncha mabacho kinaweza kuwa risasi au vipande vya vyuma vya bomu.


Mh Mbowe akiwa nyumbani kwa wazazi wa mmoja wa marehemu (Ramadhani) eneo la Mianzini kuwapa pole kwa kuondokewa na mpendwa wao.
James Ole Millya na Mbunge Lema wakimjulia hali mmoja wa majeruhi walilazwa hospitali ya Seliani

Mtoto Sharifa nae amalazwa hospitalini hapo kwa majeraha ya mlipuko
Dereva wa mgombea wa Chadema Kata ya Themi, Bw beni akiwa majeruhi kitandani

Kamanda wa Chadema ambaye alikuwa ni mlinzi wa amani (Red Brigade) katika mkutano huo, Bw Kitumbwizi akiugulia maumivu katika hospitali ya Selian alikolazwa baada ya kujeruhiwa katika mlipuko huo. Huyu amaumizwa mguu mmoja, mkononi na sehemu ya kwapani ambapo imegundulika kuwa kuna chuma ama risasi ndani ambayo imekuwa ngumu kutolewa mapaka sasa.

PICHA: USHAHIDI WA SHOO YA MWANA FA ILIVYOBUMA


King Zilla kutoka Salasala alikuepo. 


Watu wakipata chakula na vinywaji kabla ya kuingia kwenye show 


Meneja wa Ommy Dimpoz, Muba, Salama na Ommy Dimpoz. 























Ilikua ni show inayohitaji watu 400 tu
Ben Pol kwenye stage. 
FA mwenyewe. 



Mandojo na Domokaya, Kilimanjaro Band, Fa na Linah pamoja na Maua. 



Mwigizaji Wema Sepetu akiingia. 


Reuben Ncha kali na Shadee. 
Vanessa Mdee na B12