P.FUNK:MWAMBIE KUSAGA KUANZIA LEO SITAKI KUSIKIA MIKASI IKIPIGWA CLOUDS FM


Muda mfupi uliopita djchoka amepokea simu kutoka kwa Producer mkongwe hapa bongo anayejulikana kwa jina la P Fuck Majani na kumuuomba aipokee msg hii hapa chini na kuwaomba watanzania walijue hili na baadae atatoa barua rasmi. 

Mtoto wa Sokoine alipuka


MTOTO mkubwa wa Waziri Mkuu wa zamani Hayati Edward Moringe Sokoine, Lazaro Sokoine, ameibuka na kutoa madai mazito ya kutaka mwili wa baba yake ufanyiwe uchunguzi, kubaini chanzo cha kifo chake.

Mbali na kutaka uchunguzi huo, Lazaro pia amemuandikia barua Rais Jakaya Kikwete akielezea mlolongo wa matukio mengi, likiwemo mgogoro wa familia hiyo na kuporwa kwa ardhi na mali zake zingine alizoachiwa na Hayati Sokoine.

Lazaro alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam katika mahojiano maalumu na Tanzania Daima Jumatano, huku akishusha madai mazito dhidi ya Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Namelock Sokoine, ambaye ni mdogo wake.

Kwa nini mwili wa Sokoine uchunguzwe?

Akielezea sababu za kutaka mwili wa Sokoine uchunguzwe, Lazaro alisema miezi minne kabla ya kifo chake mwaka 1984 baba yake alienda nchini Cuba wakati Lazaro akiwa masomoni nchini humo; Sokoine alimwambia mwanaye huyo kuwa asishangae kusikia amekufa kwa njia yoyote ile ikiwamo kupigwa risasi kwani kuna watu wanamuwinda.

Alisema baada ya baba yake kumueleza hivyo alihoji sababu ya kuwa na hofu hiyo ambapo Sokoine alijibu kuwa hali ya nchi wakati huo chini ya Mwalimu Julius Nyerere, ilikuwa mbaya kutokana na vita dhidi ya wahujumu uchumi.

Mtoto huyo (pichani) ambaye ana hali mbaya kiuchumi, alisema baba yake aliendelea kumwambia kuwa kutokana na hali hiyo, Mwalimu Nyerere alimuongezea ulinzi kutoka askari wanne hadi 14.

“Baba alikuja Cuba kwa ajili ya sherehe za uhuru wa nchi hiyo na akaniambia maneno hayo mazito nami nikaenda kuongea na walinzi wake ambao ni Mashaka, Kimaro na Kalbert juu ya hofu hiyo ya baba,” alisema Lazaro.

Alisema miezi minne baadaye alipata taarifa ya kifo cha baba yake kupitia Ikulu ya Cuba hali iliyomfanya ayakumbuke maneno ya tahadhari aliyoambiwa juu ya hofu ya kuuawa.

Akieleza sababu nyingine iliyomfanya atake mwili wa baba yake uchunguzwe upya, Lazaro alisema agizo la Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa wa wakati huo Imran Kombe, kuwataka walinzi wa Sokoine waliokuwa Dodoma watangulie Arusha badala ya kuandamana naye kwenda jijini Dar es Salaam, linatia shaka kwamba kulikuwa na mpango wa kutaka kumuua.

Alisema kutokana na mazingira hayo, amekuwa akitamani sana kuanzisha harakati za kutaka mwili wa kiongozi huyo maarufu uchunguzwe, lakini hali yake kiuchumi ndiyo inayomkwamisha.

“Kwa sasa sina uwezo ila nikipata pesa nitaanzisha mchakato wa kuchunguza kifo cha baba yangu; nimekuwa nikiuliza hili kwa muda mrefu, watu wamenichukia na sasa wananipiga vita hadi ndani ya familia kwa kuhoji suala hilo, mdogo wangu anayeitwa Joseph Sokoine aliyeko ubalozi wa Tanzania nchini Canada aliniambia nisiulizeulize hili suala, wala nisiliingilie kwani siku moja wataning’oa macho au kuniondoa duniani,” anaongeza Lazaro.

Alisema hivi karibuni wakati mwili wa Sokoine ulipozikwa kwenye kaburi jipya kutoka lile la awali, aliiambia familia yake kwamba isifunge milango ya kaburi ili uchunguzi wa mwili wa baba ufanyike.

Hivi karibuni gazeti hili lilipata kuandika taarifa ya mwili wa Sokoine kuzikwa kwenye kaburi jipya baada ya lile la awali kuharibika na kwamba familia ina mpango wa kutaka kuufanyia uchunguzi mwili huo.

Ikumbukwe kuwa wakati wa kifo chake kulikuwa na mjadala mzito, wengi wakidai aliuawa na kwamba kifo chake kilipangwa na mahasimu wake ndani na nje ya serikali ambao walikerwa na operesheni yake ya kupambana na wahujumu uchumi na mali za taifa.

Kwa mujibu wa sheria, mwili ukishazikwa unaruhusiwa kufanyiwa uchunguzi baada ya miaka 30 na mwakani mwili wa Sokoine utafikisha umri wa miaka 30 tangu ulipozikwa na huo utakuwa muda muafaka kwa wana ndugu hao kutaka kujua ukweli wa kifo cha ndugu yao.

Madai ya kuporwa mali

Akizungumzia suala la kuporwa mali na ardhi, Lazaro alisema ameamua kumuandikia barua Rais Kikwete ili aingilie kati kupata haki zake.

Alisema mwaka 1983, akiwa nchini Cuba Sokoine alimkabidhi kiwanja katika eneo la Kunduchi na hati ya kusaini umiliki wa kiwanja hicho ilipelekwa nchini humo na Paraseko Kone, ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Singida.

Alisema baada ya kumaliza kusaini, Kone alizirejesha hati hizo na kumkabidhi aliyekuwa Mkurugenzi wa Katapila Tanzania kwa wakati huo, Victor Ole Kimesera, ambaye kwa sasa ni Katibu Mtendaji ofisi ya Katibu Mkuu CHADEMA.

Aliongeza kuwa mwaka 1984 alipokuwa kwenye msiba wa baba yake, aliulizia mahala zilipo nyaraka hizo na mama yake alimueleza zilikokuwa na kwamba alipomaliza masomo nchini Cuba alirejea nchini na kukuta kiwanja hicho kimemilikishwa kwa mdogo wake Kilimbe Edward Sokoine.

Alisema baadaye kiwanja hicho kwa kushirikiana na mdogo wake, walikiuza kwa kampuni moja (jina linahifadhiwa), bila ridhaa yake.

“Kwa sasa mimi nina matatizo makubwa hata msaada unaotolewa na serikali kwa familia yetu mimi sijawahi kuupata nakuapia hata gari wananikataza nisisogelee na anayefanya hivi ni mdogo wangu, Namelock,” alisema Lazaro na kuongeza.

“Baba aliniambia kiwanja nimekupatia na pia kuna ng’ombe dume 600 wa kutumia kujengea hicho kiwanja.”

Lazaro alisema kutokana na hali hiyo aliamua kumuandika barua Rais Kikwete Mei 13 mwaka huu na kulazimika kuja jijini Dar es Salaam kujua hatma ya barua yake kama ilishafika mikononi mwa Rais Kikwete.

“Nina mke na watoto wawili hadi hivi sasa mke wangu amerudi kwao kwa kukosa matunzo, maisha ya kulala chini na kukosa chakula yananikabili; ninaleta matatizo haya kwako ili uweze kunisaidia kupata haki zangu zilizotaifishwa ili niondokane na maisha magumu niliyonayo ya kukosa sehemu ya kulala huku nikiwa na watoto wadogo chini ya miaka mitano na kukosa pesa ya kujikimu kimaisha,” inasomeka sehemu ya barua hiyo.

Kutokana na madai hayo Tanzania Daima Jumatano iliwasiliana na Mkuu wa Mkoa wa Singida kwa simu kujua ukweli wa madai hayo.

Mkuu wa mkoa huyo alisema hakumbuki kupeleka fomu kwa Lazaro akiwa masomoni Cuba, lakini alikiri kukutana naye nchini homo.

“Nakumbuka nilikutana na kijana huyo wakati huo akiwa masomoni Cuba ila sikumbuki hilo la kumpelekea fomu ya umiliki wa kiwanja,” alisema Kone.

Kwa upande wake Namelock ambaye ni mbunge wa viti maalumu (CCM) alikiri kuwa kiwanja anachoeleza kaka yake ni haki yake na kwamba kwa sasa kinamilikiwa na watu watatu kwa njia ya ujanja.

“Tumefuatilia bila mafanikio na juzi alipoenda Ikulu nilimwambia afadhali amwandikie barua Rais, na aliandika imefika kwa kuwa msaidizi wa Rais alinipigia, tena ramani ya hicho kiwanja ninayo hadi sasa,” alisema Namelock.”

Sokoine alifariki Aprili 12, 1984 eneo la Wami-Dakawa akiwa njiani kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam

OBAMA: UTABIRI WA ULINZI UTAKAVYOKUWA ATAKAPOKUJA TANZANIA

OBAMA
ULINZI WA UHAKIA
SECURITY RING


NINJA NA COMANDOO WATAKUWEPO

WALENGA SHABAHA NA MBWA


PRESIDENTIAL LAMEZINE




















HIVYI NDIVYO OBAMA HUZINGIRWA NA WANAUSALAMA

MSTARI WA KWANZA HUKAA POLICE WA KAWAIDA, MSTARI WA PILI WANAUSALAMA KUKAGUA SILAHA



HAWA HUPANDA HATA KWENYE MAPAAA WAONE KWA MBALI 

TOCHI HIZI HUTUMIWA NA WATU SPECIAL KUCHUNGUZA KAMA KUNA GARI AU MTU MWENYE MLIPUKO KWA MBALI NA KUMZUIA HATA KABLA HAJAFIKA KARIBU NA TUKIO



HABARI ZAIDI JUU YA KIFO CHA MANGWEAR:


Ngwea akiwa na msanii M to the P jana south africa.

Kuna taarifa kuwa chanzo cha kifo cha ghafla cha rapper Mangweir ni kuzidisha madawa ya kulevya aliyotumia usiku wa kuamkia leo. 

Hussein Original ambaye yupo Pretoria amesema Ngwear na   M to the P  ambaye walikuwa room moja  wamekutwa wamezima   baada  ya  kuzidhisha  madawa  ya  kulevya...

Hata hivyo mwenyeji wa rapper Albert Mangwea aliyefariki leo jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini, amesema hit maker huyo wa Mikasi amefariki akiwa usingizini.

Akiongea na mwandishi wetu  muda mfupi uliopita, mwenyeji huyo aitwaye Jonathan amesema usiku wa kuamkia leo Mangwair alirudi nyumbani alikofikia akiwa mzima wa afya lakini mpaka kunakucha hakuonesha dalili za kuamka.


Ameongeza kuwa asubuhi kulipokucha aliondoka na  kuendela na mishemishe yake na alipokuwa huko wenzake walimpigia simu kumtaarifu kuwa wamempeleka hospitali ya St. Helen ya jijini humo kwakuwa alikuwa bado hajaamka na ndipo walipogundua kuwa ameshafariki.

Jonathan  amesema hakuweza kujua sababu za kifo cha Ngwair kwakuwa maelezo ya daktari yalikuwa kitaalam kiasi cha kushindwa kuelewa. Ngwair alikuwa amepanga kurudi leo nchini.


Taarifa za kifo cha Ngwair zimepokelewa kwa mshtuko na watu na makampuni mbalimbali nchini yametuma salamu za rambi rambi kupitia kwenye mitandao ya kijamii.


Kilimanjaro Lager ‏
Umeondoka wakati bado tasnia ya muziki inakuhitaji. Pumzika kwa Amani Albert Mangwea “Cowwizy”.


Ndovu Special Malt
R.I.P Albert Mangweir! You will be missed by many Tanzanians. 


Adam Nditi 
Yani siamini Mangwear amefariki dunia nini ilichomkuta #RIP #Mangwair #akaCowbama


Diva ‏
Jamani Ngwair , am in tears now ….. Jamani!. I can’t believe this. I can’t tweet The RIP….. Whyyyyy?

BREAKING NEWS: MWANAMUZIKI WA Hip-Hop ALBERT MANGWAIR AMEFARIKI LEO

Ngwea akiwa na msanii M to the P jana south africa.mtu wa karibu anasema walitakiwa kurudi dar leo lakini waliwakuta wamezima kwenye room wote wawili baada ya kuji overdose madawa ya kulevya na M to the P yupo hoi hospitali
BREAKING NEWS: Mwanamuziki wa Hip-Hop ALBERT MANGWAIR amefariki dunia LEO huko Afrika Kusini katika hospitali ya Hellena Joseph. Endelea kufuatilia ukurasa huu kwa habari zaidi.........

GODBLESS LEMA: MESEJI ILITOKA KWA MKUU WA MKOA

Tarehe 21 /5/2013 Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) L iberatus Sabas ambaye ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha aliongea na waandishi wa habari juu ya shutuma zangu juu ya ujumbe wa maneno mfupi niliopokea kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bwana Magessa Mulongo siku ya tarehe 25.04.2013 kutoka kwenye namba anayotumia mkuu wa Mkoa namba 0752960276 namba ambayo imesajiliwa kwa jina la Magessa Mulongo kwenda namba 0764150747 namba ambayo imesajiliwa kwa jina la Neema Lema namba ninayo tumia Mimi , ujumbe unaosema “ Umeruka kihunzi cha kwanza nitakuonyesha kuwa mimi ni Serikali , ulikojificha nitakupata na nitakupa kesi ninayotaka mimi “

Nimesikitishwa na kufedheheshwa sana na taarifa hii ambayo sasa inathibitisha bila mashaka kuwa Jeshi la Polisi Arusha hasa Mkuu wake anatumika na sina shaka kusema kuwa yeye ni KIPEPERUSHI cha Mkuu wa Mkoa , baada ya Mimi kupokea ujumbe huu tarehe 25/4/2013 nilitoa taarifa kwa vyombo vya habari na nia yangu ya kwenda mahakamani juu ya vitisho hivi .

Haya yafuatayo ni maswali ya msingi ninayojiuliza bila kupata majibu sawia kuhusu taarifa ya Jeshi la Polisi na Mtandao wa simu wa Vodacom .
1) Kwani nini Jeshi la Polisi walikataa kuchukua maelezo yangu Mimi juu ya tuhuma hizo nzito dhidi ya Mkuu wa Mkoa ambaye amenitumia meseji kupitia simu yake ya mkononi kama ninavyolalamika ? lakini pia ni muda takribani mwezi umepita tangu nimetoa malalamiko yangu je katika kipindi chote cha mwezi mzima Jeshi la Polisi waliona ni busara kwenda Kampuni ya Vodacom kutafuta mawasiliano yangu na Mkuu wa Mkoa bila hata kuchukuwa maelezo ya mlalamikaji ambaye pia kwa nafasi yake katika Jamii ni Mbunge ?

2) Nilipokuwa rumande Msaidizi wa Mkuu wa Makosa ya Upelelezi Arusha alinifuata na kuniomba nimpe simu yangu, nilimwambia sina nimemwachia Mke wangu na walimtafuta Mke wangu na kumuomba hiyo simu na kumuhakikishia kuwa akiwapa simu wataniachia na kunifutia kesi na Mke wangu aliwajibu kuwa simu alidondosha kwenye gari ya Polisi ile ambayo walinichukua nayo usiku wa siku waliyonikamata , waliita ile gari wakatafuta hiyo simu na walipokosa walichukua pochi ya Mke wangu na kumwaga vitu vyote na kuanza kuitafuta simu na kumpekua , Je Polisi hapa walikuwa wamekusudia nini ?

3) Kwa namna ya kawaida sana ya upelelezi baada ya Polisi na Vodacom kukuta simu ninayotumia imesajiliwa kwa jina lingine katika msingi wa kawaida wa utafiti Kama ambavyo naelewa au kufikiri vyema huyu mwenye Jina hili angetafutwa kwani meseji ilionekana imetoka kwa Magessa Mulongo na imekwenda kwa Neema Lema , lakini aliyekuwa analalamika ni Godbless Lema , je kama Polisi sio Kipeperushi cha Serikali walipata wapi ujasiri wakutoa maelezo waliyotoa wakati kwenye usajili wa mitandao ya simu namba 0764150747 imesajiliwa kwa jina la Neema Lema bila hata kuchukua nafasi ya kumtafuta Neema Lem a kujua ni nani huyo ambaye simu yake inatumiwa na Mtu mwingine ? na ni kwanini Polisi hawakusema kuwa mimi nimedanganya kwani namba hiyo sio yangu ni ya Neema Lema ?

4) Mimi kama mteja ni nayetumia namba 0764150747 nimehiifadhi namba ya Magesa Mulongo 0752960276 kama ( RC ARUSHA VODA) na ndio jina lililokuja na ujumbe wa vitisho katika simu ninayotumia . Vile vile katika barua ya Vodacom kuna maelelzo ambayo ni ya mashaka , kwamba namba ya simu ya Magesa Mulongo ilituma meseji kwenda namba 0764150747 yenye usajili wa jina la Neema Lema kuwa ni kweli kuwa meseji ilitumwa na namba ya Mulongo isipokuwa Center number sio ya Vodacom , swali , kama namba ya Mulongo ni ya Kampuni yao ndio iliyotuma meseji basi hata hiyo center number ni ya kwao kwani kama ingekuwa sio ya kwao Kampuni ya Vodacom isingeweza kuona taarifa zake katika mfumo wake wa mawasiliano na kuzitolea taarifa hivyo kama wameweza kuwa na taarifa zake maana yake ni kuwa mawasiliano hayo yamepita katika mitandao yao ndio maana Kampuni ya Vodacom imepata taarifa za mawasiliano haya na kuyathibitisha kwa Polisi bila hata Kampuni yenyewe kuchuka nafasi ya kumtafuta mlalamikaji na kujua nini kilichotokea kwenye simu yake , lakini vile vile mimi kama mteja sina wakati wa kukagua center number pindi napotumia simu yangu na sijawahi kufanya hivyo na wala sijawahi kuzingatia kwani sio wajibu muhimu katika matumizi ya simu yangu ya mkononi.

5) Wakati Polisi walipoita vyombo vya habari dhana muhimu hapa ilikuwa ni kutaka kumsafisha Mkuu wa Mkoa na ndio maana barua ya Vodacom kwenda Polisi iko kwenye mitandao ya kijamii jambo mabalo Polisi au Vodacom wasingepeswa kufanya hivyo kama kungekuwa hakuna malengo ya kisiasa katika taarifa hii lakini kitendo cha Polisi cha kutoa taarifa bila kuona meseji kutoka katika simu ninayotumia huu ni uhuni mwingine ambapo ni wa msingi kwa Jeshi la Polisi kwani taarifa zinaonyesha kuwa Polisi wote ambao wamekuwa watesaji na waonevu kwa Viongozi wa Upinzani wamekuwa wakipanda vyeo na kupata thamani kubwa machoni kwa Watawala dhalimu na mifano halisi ya wazi iko mingi.

6) Ni dhahiri kwamba zinatumika njia nyingi kumsafisha Mkuu wa Mkoa kwa masilahi ya Serikali . Katika kesi ya uzushi niliyofunguliwa na Polisi ujumbe huu wa meseji utatumika kama ushaidi na mahakama itaona na kufafanua ukweli halisi , hivyo wote wanoangaika wasubiri kwani hivi punde tutakutana mahakamani .

GODBLESS J LEMA ( MP)

26/5/2013

Lipumba akiri kumsaidia Kikwete Uchaguzi 2010

LIPUMBA AIBUA JAMBO ZITO - AKIRI KUMNUSURU KIKWETE UCHAGUZI MKUU MWAKA 2010

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ameibua suala zito akikihusisha chama chake na “kumnusuru” Rais Jakaya Kikwete katika uchaguzi mkuu uliopita.

Profesa Lipumba alitoboa siri hiyo katika Msikiti wa Idrissa, Kariakoo, jijini Dar es Salaam, alikokwenda kuswali swala ya Ijumaa.

Huku akisisitiza juu ya umuhimu wa mshikamano wa kiimani, Profesa Lipumba alianza kwa kuzungumzia matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2010, na ushindani mkali wa kisiasa uliokuwapo.

Alisema hawaoni matunda ya jitihada walizofanya kumnusuru Rais Kikwete asishindwe, kwani hata chini ya uongozi wake, Waislamu wameendelea kutothaminiwa.

“Ninyi masheikh mnajua vizuri zaidi hali ya kisiasa ilivyokuwa, kwamba ilibidi zifanyike juhudi za makusudi ili kuokoa jahazi. Lakini pamoja na kuliokoa jahazi, hali halisi inaonyesha mpaka sasa hakuna matunda yoyote yaliyopatikana, na tupo katika mtihani mgumu zaidi,” alisema.

Katika hali ambayo inasemekana ushindi wa Rais Kikwete ulipatikana kwa mbinu, huku wengine wakiituhumu Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa ilimnusuru mgombea wa CCM, kauli hii ya Profesa Lipumba inadokeza kwamba anajua mkakati zaidi wa kazi ya Tume ya Uchaguzi.

Katika hali isiyo ya kawaida, Profesa Lipumba anaonekana kuhamasisha Waislamu kujipanga akisema “wenzetu wameanza kujipanga” kuelekea 2015.

“Kwahiyo kama Waislamu tunataka kupata haki zetu, kama tunataka kuishi kama raia wa daraja la kwanza katika nchi yetu, lazima tujipange kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015; na sisi tuanze kujipanga kwa sababu wenzetu wameanza kujipanga, vinginevyo tutaendelea kubaki maskini na raia wa daraja la nne katika nchi yetu wenyewe.

“Mwaka 2010 wakati mshindi wa uchaguzi wa rais alipotangazwa, mimi nilikwenda kwenye hafla ya kutangazwa matokeo, na nilikwenda makusudi tu, siyo kwamba uchaguzi ulikuwa huru na wa haki, ila nilikwenda makusudi kwa kujua hali ya kisiasa ilivyokuwa wakati huo.

“Huku nilikutana na Sheikh Basaleh. Nilipokutana naye, alinipongeza; sijui kama yeye anakumbuka, akaniambia ‘umeweka mbele imani yako na umekuwa mwelewa wa mambo.’”

Hata hivyo, licha ya Profesa Lipumba kuwaambia Waislamu wajipange kwa ajili ya uchaguzi mkuu, hakusema wajipange kupitia chama kipi.

Lakini alisisitiza kwamba uchaguzi ujao ni zaidi ya siasa au rais yupi anafaa, bali maslahi, hasa ya rasilimali nyeti zinazopatikana katika ukanda wa Pwani ya Mashariki, eneo ambalo alisema linakaliwa zaidi na watu wenye imani ya Kiislamu.

Katika moja ya kauli zake, Profesa Lipumba alisema kwamba kuna chama kimoja kinataka kuchukua madaraka ya nchi, lakini kinasaidiwa na mataifa ya magharibi, yasiyoenzi wala kuthamini imani ya Kiislamu.

Kwa muda sasa, zimekuwapo tetesi kwamba CCM imekuwa inafanya siasa za udini dhidi ya vyama vya upinzani, hasa inapoona maslahi yake yapo hatarini.

Mwaka 2010 makada kadhaa wa CCM walitumia mitandao ya simu kuchonga (spoofing) ujumbe wa simu ulioshambulia mgombea mmoja wa upinzani, ukimhusisha na imani yake.

Kauli ya Lipumba imethibitisha pia minong’ono iliyokuwapo muda mrefu kuwa baadhi ya kura za Profesa Lipumba zilipotelea kwa Rais Kikwete.

Katika uchaguzi huo, Lipumba alitangazwa kushika namba ya tatu, nyuma ya Rais Kikwete na Dk. Willibrod Slaa wa CHADEMA.

Alipoulizwa kuhusu ziara yake msikitini na kauli aliyotoa, Profesa Lipumba alikiri kwamba alikwenda kuzungumzia hali ya kisiasa nchini

SIRI YA KIFO CHA KAMANDA WA POLISI LIBERATUS BARLOW YAFICHUKA.

Sasa ni wazi kwamba aliyekuwa kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza ameuawa na genge ndani ya Polisi akiwemo Kamanda Polisi anayejulikana kwa jina la Muna, gazeti la Jamhuri limeripoti katika ukurasa wa Mbele kabisa (Nimesoma kwenye website yao Deo Balile akilalamika gazeti kununuliwa kwa jumla na watu wasiojulikana) 

Kuvuja kwa siri hiyo kumetokana na mmoja wa jambazi sugu ajulikanaye kwa jina la Edward Malele kujisalimisha ktk vyombo vya ulinzi na kutoa siri zote. 

Jambazi huyu aliombwa wa genge ndani ya polisi kushiriki katika mpango wa kumwua kamanda Barlow. Akakataa kwa kuwa aliwahi kumfahamu kwa karibu kamanda Barlow. 

Baada ya kukataa kutekeleza agizo hilo baada ya siku chache alishtakiwa kwa kosa la ujambazi na kuswekwa Rumande.

Akiwa huko ndani ya wiki moja alisikia habari za kifo cha kamanda Barlow. Akajua akina na Muna aliowakatalia wamefanya kazi aliyoikataa yeye. Na alijua yuko mahabusu kwa sababu ya kukataa mradi huo.

Baada ya kukaa huko muda mrefu bila shitaka kueleweka wala mshataki wake huko Lupango walimua kumwaichia. Akagoma kutoka kwa sababu anajua kuwa, kwa kuwa amepelekwa huko ili kuficha siri hivyo, akitoka lazima atauawa. Baada ya muda akaamua kukubali kutoka lupango na kukimbilia kituo cha JWTZ huko Mwanza. 

Huko JWTZ Alijieleza vya kutosha na wanajeshi walimwonea huruma wakampa Nauli na Tsh 10,000/= ya kula njiani ilie aende Bungeni huku wakiwa wamemkabidhi namba za simu za wabunge 2 wa upinzani ili wamsaidie. 

Kutokana na kutokuelewa kwake alipokuwa anashangaa shangaa katika eneo la Bunge, alikamatwa na polisi wanalinda eneo hilo. Polisi hao wakapiga simu Dodoma central na Mwanza. Haraka haraka mwanza wakataka arudishwe mwanza kwa kuwa ni jambazi sugu. 

Hata hivyo, kwa katika kurupushani hiyo taarifa zimeshameshamfikia Pinda na Nchimbi ambapo gazeti linaripoti kuwa Pinda ameagiza kijana huyo apewe ulinzi na asirudishwe Mwanza.

Hata hivyo amepelekwa kusiko julikana. 

Kwa mapana zaidi soma gazeti la Jamhuri KAMA zinanunuliwa kwa kasi na watu wasiofahamika

SOURCE: JAMIIFORUMS

PROFESA JAY: AJIUNGA CHADEMA:

Rapper mkongwe nchini, Joseph Haule aka Profesa Jay amejiunga rasmi na Chama cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA.




Profesa amekabidhiwa kadi ya uanachama wa CHADEMA na mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi aka Sugu. 


Kujiunga rasmi kwa Profesa kwenye chama hicho kunaashiria kuwa huenda akawa na nia ya kugombea ubunge kwa tiketi ya chama hicho mwaka 2015.
Profesa ameamua kuweka wazi uamuzi wake baada ya watu wengi kuanza kumuuliza maswali. “Mmeniuliza sana kwamba mimi ni CHAMA gani jibu litapatikana Muda sio mrefu!! Still in Dodoma STAY TUNED,” alitweet.
Rapper huyo anayejulikana kama mchawi wa rhymes yupo Dodoma pamoja na wasanii wengine akiwemo Lady Jaydee kwa mwaliko wa Sugu

PICHA ZA MBUNGE MSIGWA ALIVYOFIKISHWA MAHAKAMANI IRINGA MCHANA




Mbunge Msigwa akishuka katika gari ya polisi baada ya kufikishwa mahakamani mchana huu



Mbunge Msigwa akishuka katika gari hilo la polisi tayari kwa kuelekea chumba cha mahakama



Mbunge Msigwa akiwa na gazeti mkononi baada ya kufikishwa mahakamani leo



Watuhumiwa wengine wa vurugu za machinga na polisi wakishuka katika karandinga la polisi










Wakili wa Msigwa kulia akiteta jambo nje ya mahakama



Kada wa Chadema Frank Mwaisumbe akiingia na viongozi wengine wa chadema mahakamani hapo huku wafuasi wao wakizuiwa nje ya mahakama



Wafuasi wa Chadema wakiwa wamezuiliwa nje ya viwanja vya mahakama kuu kanda ya Iringa wakati mbunge alipofikishwa katika mahakamani mchana huu



Ulinzi mkali kweli kweli ..NA FRANCIS GODWIN