MBOWE ATEMBELEA ENEO LA MLIPUKO, PAMOJA NA KUTEMBELEA FAMILIA ZA WAFIWA NA MAJERUHI WA MABOMU NA RISASI ARUSHA


Mwenyekiti wa Chadema, Mh freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini Mh Godbless Lema wakiwa katika uwanja wa Soweto mchana wa leo wakati zoezi la kuchukua vipimo mbalimbali likiendelea chini ya usimamizi wa wataalamu toka Jeshini.

Mbowe na Lema wakishauriana jambo..
Eneo la maafa. Inaelezwa kuwa wataalamu wa jeshi waligundua kuwako kwa kitu ndani ya tanki la mafuta na hivyo kuamua kulikata. Taarifa hizo zinadai kwamba kulikuwa na mabomu yametegwa chini ya gari na hivyo tank hilo lilishmabuliwa kwa risasi labda utokee mlipuko! Pia gari hii ya amatangazo ina majeraha mawili mlango wa kushoto yaliyotokana na kitu chenye ncha mabacho kinaweza kuwa risasi au vipande vya vyuma vya bomu.


Mh Mbowe akiwa nyumbani kwa wazazi wa mmoja wa marehemu (Ramadhani) eneo la Mianzini kuwapa pole kwa kuondokewa na mpendwa wao.
James Ole Millya na Mbunge Lema wakimjulia hali mmoja wa majeruhi walilazwa hospitali ya Seliani

Mtoto Sharifa nae amalazwa hospitalini hapo kwa majeraha ya mlipuko
Dereva wa mgombea wa Chadema Kata ya Themi, Bw beni akiwa majeruhi kitandani

Kamanda wa Chadema ambaye alikuwa ni mlinzi wa amani (Red Brigade) katika mkutano huo, Bw Kitumbwizi akiugulia maumivu katika hospitali ya Selian alikolazwa baada ya kujeruhiwa katika mlipuko huo. Huyu amaumizwa mguu mmoja, mkononi na sehemu ya kwapani ambapo imegundulika kuwa kuna chuma ama risasi ndani ambayo imekuwa ngumu kutolewa mapaka sasa.